Posts

Showing posts from November 30, 2015

KIMENUKA..Miss Tanzania Atajwa Ufisadi wa Sh1.3 Trilioni

Image
  Aliyekuwa ofisa mwandamizi wa benki ya Stanbic tawi la Tanzania, Shose Sinare amehusishwa na mipango ya kifisadi ambayo imeisababishia Serikali ya Tanzania hasara ya Sh1.3 trilioni kati ya mwaka 2012 na 2013. Taarifa ambazo gazeti hili limepata kutoka Uingereza na hapa nchini, mwanadada huyo ambaye alikuwa mrembo wa Tanzania mwaka 1996, alishirikiana na aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bashir Awale. Sinare hakupatikana kufafanua suala hilo ilhali Awale alifukuzwa nchini hivi karibuni. Alipoulizwa jana kuhusu tuhuma hizo, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hosea alisema anatambua suala hilo,  linafuatiliwa na taasisi yake na hakutaka kutoa maelezo zaidi. Taarifa kwamba Serikali imetumbukia katika kashfa nyingine kubwa ya ufisadi zimebainika baada Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Ufisadi ya Uingereza (SFO) kuwasilisha mahakamani ushahidi wake kwamba kiasi cha Sh1.3 trilioni kilipotea wakati wa uuzwaji wa hati fungani za Serikali kwa benki ya Stan...

Kimbunga cha Magufuli chatua Mashirika ya Umma, ATCL, TRL And Tazara Matumbo Moto

Image
Msajili wa Hazina, Lawrence Mafuru amezitaka taasisi na mashirika ya umma nchini kuacha utegemezi kwa Serikali, badala yake kupunguza matumizi na wafanyakazi ili kuongeza mapato na ufanisi. Mafuru alisema Serikali imebeba mzigo wa taasisi na mashirika hayo kwa kutegemea izipatia fedha kutoka Hazina kwa ajili ya kujiendesha, na kulipa mishahara ya wafanyakazi na kusababisha ufanisi wao kuwa mdogo. Mafuru pia alitangaza kufuta posho za wabunge katika bodi za mashirika na kuanzisha mchakato wa kuwaondoa katika mashirika hayo, ili wabaki na jukumu lao la msingi la kuikosoa Serikali badala ya kuingia katika utendaji. Kuhusu uzalishaji Msajili huyo alisema inashangaza kuona kwamba mpaka sasa kuna mashirika ya umma ambayo bado yanaitegemea Serikali kulipa mishahara ya wafanyakazi wake. Aliyataja mashirika hayo kuwa ni Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), Kampuni ya Hifadhi za Reli (RAHCO) na Mamlaka ya Reli Tanzania na Zambia (Tazara). Alisema hakuna h...

Je Kasi ya Magufuli na Watendaji Wake Ndio Mwanzo wa Udikteta? Ama ni Kasi Inayotakiwa Katika Taifa Hili ?

Image
Mwalimu Nyerere once a time alisema kama nigetaka kuwa dicteta ningeweza. hivi sasa watanzania tumepata upofu wala hatuoni tena. nimewahi kusema kwenye post zangu kuwa IPO siku watanzania watamkumbuka Rais Kikwete. kwanini niseme ivo, twende pamoja na kama unamatongotongo kanawe,na kama umemeza viroba kaa mbali na hii post,only great thinkers. 1. VITISHO NA HOFU ukubali au ukatae magufuli sasa anaogopwa na amejaza hofu wananchi haswa wafanyakazi na wafanyabiashara. kumbekeni Adolph Hitler alishinda uchaguzi wala hakupindua serikali pia alipata public sympathy hata pale alipokesea. tazama sasa hata hii post kuna watu watakosoa bila kujali relevance yake. 2. KUVUNJWA KWA HAKI ZA BINADAMU. hivi sasa unaweza kuweka polisi bila kushtakiwa mfano. hivi jeuri ya Paul Makonda yakumweka MTU kizuizini bila kumpeleka mahakamani ni uvunjaji wa haki za binadamu. sasa ivi kila mkuu wa wilaya anaamua tu kwa ubabe hats bila kuangalia haki za binadamu. 3.KUVUNJWA KWA UTAWALA WA SHERI...

Sakata la Makontena: Mwigulu, Saada Mkuya, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Wanatakiwa Wawe Ndani

Image
Ni jambo la kusikitisha kuwepo upotevu wa kiasi kikubwa cha pesa kwa ukwepaji kodi wa makontainer 349 yenye thamani billion 80 wakati wenye dhamana ya kulinda mali hizi zisipotee wakina Mwigulu Nchemba, Saada Mkuya, Katibu Mkuu wizara ya fedha wakiwa nje bila kuchukuliwa na hatua yoyote kama walivyo wenzao sita walioachishwa kazi na kuwekwa chini ya uchunguzi, haiwezekani makontiner idadi kubwa kama hii ipotee billa wakuu hawa kujua lolote, tunaiomba serikali iwafuatilia na kuwawajibisha mara moja, hivyo hivyo katika uongozi wako Mh. Tingtinga untakiwa kuwafyeka wote. Vivyo hivyo tnataka taarifa sahii ya maandishi kuonyesha kama fedha zlizoamriwa kulipwa kutoka kwa wana-ESCROW kama zimelipwa kwa wakati. Jamii Forums

Taarifa Kutoka Azam Kampuni ya Bakhresa Kuhusu Kuhusishwa Kwnye Makontena 349 Yaliyotolewa Bandarini Bila Kulipiwa Ushuru

Image
Kumekuwa na taarifa zinazosambazwa katika mitandao ya kijamii kuwa kampuni ya Bakhresa inahusika na upotevu wa Makontena 349 yaliyoripotiwa hivi karibuni kuwa yametolewa bandarini bila kulipiwa ushuru. Taarifa hizo zilitolewa na Waziri Mkuu wakati wa ziara yake ya Bandari ya Dar es salaam hivi karibuni. Uchunguzi wetu umeonyesha kuwa si kweli kuwa kuna makontena yenye bidhaa zilizoingizwa na kampuni hio ama ni miongoni mwa makontena yaliyohusika katika sakata hilo. Isipokuwa kumetokea upotevu wa makontena yaliyoingizwa nchini na baadhi ya wafanyabiashara katika eneo la kuhifadhia makontena(ICD) linalomilikiwa na kampuni hiyo la Azam ICD. Aidha imebainika kuwa kuna uchunguzi unaofanywa na mamlaka ya mapato nchini TRA, huku kukiwa na ushirikiano na uongozi wa Kampuni hiyo (SSB Group of Companies) kuhakikisha wale wote wanaohusika na upotevu huo wanachukuliwa hatua na kodi yote ya serikali inalipwa na wamiliki wote wa makontena yaliyohusika katika upotevu huo wanawajibish...
Image
M/Kiti CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe akifatana na alikuwa mgombea urais wa chama hicho Mhe. Edward Lowassa pamoja na viongozi mbalimbali wakitazama eneo ambalo Alphonce Mawazo alifanyiwa kitendo ya kinyama cha kukatwakatwa mapanga na watu wanaosemekana ni wafuasi wa CCM ikiwa ni umbali mchache kutoka kutuo cha polisi na ofisi za CCM katika barabara kuu inayoelekea Geita kutokea Busanda.

Waziri Mkuu: Tumedhamiria Kuwatumikia Watanzania...Tutahakikisha Mapato Ya Taifa Yanatumika Kwa Maslahi ya Watanzania Wote

Image
WAZIRI MKUU Majaliwa Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuhakikisha kila kinachokusanywa kama mapato ya nchi kinatumika kwa maslahi ya Watanzania wote na si kwa manufaa ya wachache. Alitoa kauli hiyo jana mchana (Jumapili, Novemba 29, 2015) wakati akifunga maadhimisho ya miaka 20 ya Dayosisi ya Pwani ya Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) kwenye ukumbi wa PTA, viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. “Serikali imeanza kukabiliana na upotevu wa mapato ya Serikali na kuepuka matumizi yasiyo ya lazima ya fedha za umma. Nia yetu ni kuhakikisha kila kinachopaswa kukusanywa kama mapato ya nchi, kikusanywe na kitumike kwa masuala ya msingi kwa ustawi wa Watanzania wote na si kwa watu wachache,” alisema. Akifunga maadhimisho hayo kwa niaba ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Waziri Mkuu alisema Serikali imedhamiria kupambana na maovu yote na kuondoa kero zinazowaumiza wananchi wa kawaida.  “Wako watu wanaoamini kwamba hatuwezi, nawa...

Moto Wa Magufuli Watua Kwa Bakhresa.......TRA Yazuia Makontena Yake Bandari Kavu, Kampuni Yake Yahusishwa na Ukwepaji Kodi

Image
KAMPUNI ya Said Salim Bakhresa (SSB) inachunguzwa na vyombo vya dola kwa tuhuma za kushiriki kukwepa kodi na hivyo kuikosesha serikali mabilioni ya fedha kutokana na makontena yaliyohifadhiwa kwenye bandari yake ya nchi kavu (ICD) ‘kupotea’ bila kulipiwa kodi.  Tayari Mamlaka ya Mapato (TRA) imepiga marufuku SSB kuingiza makontena katika bandari hiyo kavu ambako ndiko kunadaiwa kufanyika kwa vitendo hivyo vya ukwepaji wa kodi kutokana na baadhi ya makontena kupotea katika mazingira ya kutatanisha. Katika barua iliyoandikwa kwenda kwa Meneja Mkuu wa SSB iliyosainiwa na Wolfgang Salia kwa niaba ya Kamishna wa Ushuru na Forodha wa TRA, inaeleza kuwa usitishwaji huo unatokana na kampuni hiyo ya Bakhresa kuchunguzwa kwa tuhuma za kuwepo madai ya kujihusisha na ukwepaji wa kodi kwa baadhi ya kontena zilizoingia na kutoka kwenye ICD yake. Kwa mujibu wa barua hiyo, vitendo hivyo vya ukwepaji wa kodi vimefanywa kinyume cha Sheria ya Ushuru wa Pamoja wa Nchi za Jumuiya ya Afrik...

Zitto Afunguka..Asema Nguvu ya Lowassa ilikuwa Kubwa Sana Kiasi cha Kuwavurugia ACT Wazalendo Katika Uchaguzi

Image
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amesema nguvu ya aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa ilivuruga mpango wake wa kupokea wabunge 50 kabla ya Uchaguzi Mkuu. Alisema Lowassa aliyekuwa akiungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) alikuwa na nguvu kubwa kiasi cha kufanya ACT pia ishindwe kupata wabunge wengi katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika nchini Oktoba 25. Zitto alitoa kauli hiyo alipotakiwa kueleza sababu za ACT kushindwa kutimiza azma yake ya kupokea wabunge 50 kutoka vyama mbalimbali, kabla ya Uchaguzi Mkuu na kupata wabunge wengi baada ya uchaguzi huo kama alivyoahidi miezi michache kabla ya kuanza kwa kampeni. Alibainisha kuwa chama chake kilifanya mazungumzo na wabunge wengi waliokuwa CCM na Chadema ambao walikubali kujiunga nacho na kushiriki uchaguzi kupitia chama hicho. Lakini mpango huo ulibadilika baada ya Lowassa kujiunga na Chadema na baadaye kuwania urais akiungwa mkono na Ukawa. “Wabunge wengi w...

Zari wa Diamond na Mama Diamond ni Vita Kwa Kwenda Mbele....Mama Hamtaki Mkwe, Zari Atoa Masharti

Image
NI vita! Baada ya staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwenda nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’ kumwangukia mzazi mwenzake, Zarinah Hassan ‘Zari’ kufuatia kuwepo kwa figisufigisu kati yao huku mama wa msanii huyo, Sanura Kassim ‘Sandra’ akihusishwa, mazito yameibuka. TUJIUNGE NA CHANZO Habari kutoka chanzo cha ndani ya familia ya Diamond zinamwagika kwamba, Zari amekubali kuja Bongo lakini akatoa sharti: “Nakuja Bongo, Desemba 8, lakini mama (mama mkwe) aondoke pale nyumbani (Tegeta-Madale, Dar).” ZARI ATIA NGUMU, AKUBALI Chanzo hicho kilimwaga ‘ubuyu’ kwamba, awali Zari alimtilia ngumu Diamond lakini baadaye alikubali kurejesha amani kama ilivyokuwa zamani hivyo watakuja wote Bongo baada ya kujiachia vya kutoka huko Sauzi nyumbani kwa mwanadada huyo. DIAMOND KICHEKO SAUZI Kuhusu kuweka mambo sawa na kuwa atarejea Bongo na Zari na mtoto wao, Latiffah ‘Tiffah’, Diamond alilidokeza gazeti hili kwamba, sasa ni ‘full’ kicheko na anamshukuru Mungu kwa kufanikisha kufanya mambo...

Rais John Magufuli na Waziri Mkuu Majaliwa Wamuibukia Samia Suluhu Hassan Ofisini Kwake

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli (kushoto) akiagana na Makamu wake, Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati) na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa (kulia) baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Nov 30, 2015. Wa pili (kulia) ni Naibu Katibu wa Makamu wa Rais, Mohamed Khamis Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, (kushoto) akizungumza na Makamu wake, Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati) na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa, wakati Rais na Waziri Mkuu walipomtembelea Makamu Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Nov 30, 2015 kwa mazungumzo. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, (kushoto) akizungumza na Makamu wake, Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati) na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa, wakati Rais na Waziri Mkuu walipomtembelea Makamu Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Nov 30, 2015 kwa mazungumz ...

Zitto Kabwe Ayafungukia Makampuni Makubwa Tanzania Ambayo Yanakwepa Kodi....

Image
By Zitto Kabwe Kutoka Hotuba ya Waziri Mkuu 26.08.2011 – Makampuni yanayoogoza kwa kulipa kodi Note: (Highlights) Only one Mining company (the smallest i.e. - Resolute Mining), only one telecom company(Airtel Tanzania). Household names like:  MeTL, Bakhresa/Azam, IPP, VodaCom, Coca cola, Pepsi(SABCO), Serengeti Breweries, Barrick Gold, ACACIA, AngloGold Ashanti not seen. No oil marketing companies pia. One can conclude that, TBL is the most profitable company in Tanzania, NMB is the most profitable Bank. A public debate is needed. Hili ni tatizo kubwa. Here under is the an extract from the Prime Minister speech; Sehemu ndogo ya hotuba ya Waziri mkuu. Mheshimiwa Spika, 1. Nitumie nafasi hii kuwapongeza baadhi ya Walipakodi Wakubwa kwa Serikali na ambao wamefanya vizuri kati ya kipindi cha mwaka 2005 na 2011. Kwa kipindi hicho, Makampuni yaliyoongoza kwa kulipa kodi ni pamoja na: Tanzania Breweries Ltd. (Tshs 165.4b) National Microfinance Bank ...

Upotevu wa Makontena 349 Bandarini: Watu 12 Watiwa Mbaroni na Jeshi la Polisi

Image
Kufuatia agizo la Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa la kuwataka watuhumiwa wa wizi wa makontena 329 katika bandari ya Dar es salaam kuchukuliwa hatua na Jeshi la Polisi, tayari Jeshi hilo limewashikilia watuhumiwa kumi na mbili wanaohusika na wizi huo. Akiongea na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam,  Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (CP) Diwani Athumani amesema kuwa, uchunguzi unaofanywa na wataalamu waliobobea katika makosa ya uhalifu wa kifedha umeweza kuwabaini watu kumi na mbili  ambao wamehusika na wizi huo. “Kati ya watuhumiwa hao kumi na mbili, watano wanashikiliwa na Jeshi la Polisi na saba bado wapo katika upepelezi na upelelezi utakapokamilika watafikishwa mahakamani,” alisema Kamanda Athumani. Wanaoshikiliwa kutokana na tuhuma mbalimbali ni Kamishna wa Idara ya Forodha na Ushuru TRA Bw. Tiagi Masamaki, Meneja Kitengo cha Huduma za Ushuru  na Bi.  Habib Mponezia, Msimamizi Mkuu wa Kitengo cha Ushuru wa Forodha. Watuhum...

Unajua Athari za Kuitana Sweet, Dear na Baby Kwa Watu Ambao Sio Wachumba ama Mke na Mume?

Image
BABY ni neno la Kiingereza lenye maana ya mtoto, tena mara nyingi linatumika kwa mtoto mdogo. Pia lina maana nyingine ya mpenzi. Ni neno maarufu sana siku hizi; hata wazee kabisa, utasikia wanaitana baby! Mbali na hilo, yapo maneno mengine kama sweet, dear, honey na mengine mengi. Maneno yote hayo ya Kiingereza, yana maana zaidi ya moja, lakini kubwa zaidi ni kumaanisha mpenzi, mpendwa (hutumika katika kuonesha mapenzi ya dhati kwa mwingine). Leo nataka kukupa kitu kipya kabisa kichwani mwako. Unahitaji utulivu wa hali ya juu ili kujifunza hili. Ni maneno mazuri sana, ya kipekee lakini kwa upande mwingine ni hatari kwa sababu hukaribisha matatizo ambayo hayakutarajiwa na mtumiaji. HUTUMIKA WAPI HASA? “Dear, naomba uniamshe saa 12:00 asubuhi, kesho nina vikao vingi sana asubuhi,” inaweza kuwa kauli ya mume akimwambia mkewe, ambaye naye anamjibu: “Sawa sweet, usijali.” Kwa hakika ndipo sehemu sahihi zaidi kutumika. Ni maneno yenye mshawasha mkubwa na huonesha penzi la dhati...

Madhara ya Kutofanya Tendo la Ndoa Muda Mrefu.

Image
Habari zenu, nimeona niwaletee hili nina imani mtajifunza hasa kwa wale wasiofahamu,Ukikaa Muda Mrefu bila Kufanya tendo la Ndoa madhara yake ni kama haya: • Hasira za mara kwa mara katika mambo madogo, • kupendelea sana kuangalia picha za uchi, • Kusahausahau, • Kupendelea story za mapenzi, • Kutokwa damu nyingi wakati wa hedhi (Mke), • Kupenda kurukiarukia mambo ya watu wengine (tabia ya kufuatilia mambo yasiyokuhusu), • Kuumwa na kichwa, • Kukakamaa mgongo (wanaume), • Kuingiliwa kirahisi na jini mahaba, • Kupoteza umakini ktk kazi (efficiency), • Siku ukikutana kimwili na mwenye virusi bila kinga utaambukizwa kirahisi mno, • Waweza ku-develop tabia mpya ambayo hukuwahi kuwa nayo ili iwe mbadala kama ulevi n.k.

JAMAA AUA WATU WATATU AKIWEMO MKE WAKE KISA MKE KUDAI AMEOKOKA HATAKI TENA MAPENZI

Image
Polisi mkoani Ruvuma inamshikilia Amani Hyera (42), mkazi wa kijiji cha Kikunja wilayani Songea kwa tuhuma za kuwaua watu watatu. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Mihayo Msikhela, alisema tukio hilo limetokea juzi. Alisema siku ya tukio Mkuu wa polisi wa Wilaya ya Songea akiwa ofisini kwake, alipokea taarifa ya mauaji ya watu watatu. Alisema anayedaiwa kufanya mauaji hayo ni Hyera, mkazi wa kijiji cha Kikunja. Alisema mtu huyo anadaiwa kuwaua watoto wawili na mama yao kwa kuwakatakata mapanga kwa kile kilichosadikiwa kuwa ni wivu wa mapenzi. Alisema baada ya kufanya mauaji hayo, alijaribu kujiua kwa kujikata na panga shingoni, lakini hakufanikiwa kutokana na wananchi kufika kwenye eneo hilo la tukio na kumdhibiti. Kamanda Msikhela alisema mtuhumiwa anaendelea kupata matibabu na taratibu za kisheria zinafuata mara tu baada ya afya yake kuimarika. Aliwataja waliouawa katika tukio hilo kuwa ni Ester Kadege (48), ambaye ni mama mzazi wa wat...

JACKLINE olper Ajitapa Kukwapua Waume za Watu

Image
MREMBO anayesukuma maisha yake kupitia sinema Bongo, Jacqueline Wolper amejitapa kuwa haoni tatizo kuchukua mume wa mtu kwani wanaoibiwa ni wadhaifu. Akifafanua kauli yake, Wolper alisema, kumekuwa na malalamiko mengi ya mastaa wa kike kuhusu kuibiana mabwana kitu ambacho yeye anaamini kwamba kama ukiwa mbunifu huwezi kuibiwa, wanaoibiwa wasilalamike. “Bibi eeeh acha waseme. Mimi nikikuibia bwana ujue nimekuzidi ujanja inabidi uwe tu mpole siy

Mafikizolo wamjibu shabiki mwenye hasira,kuhusu kufanyika kwa video yao na Diamond Platnumz,Dec 10

Image
Kundi la Mafikizolo kutoka Africa Kusini limethibitisha kuwa lina mpango wakufanya video ya collabo yao na Diamond Platnumz December 10 2015. Uthibitisho huu umefanywa na msanii wa Mafikizolo ‘Nhlanhla Nciza’ baada ya kuulizwa na shabiki mwenye hasira kuhusu Collabo yao na Daimond Platnumz.  

TAARIFA SAHIHI KUHUSU MABUNDA YA NOTI KWENYE NDOO ZINAZENDELEA KUZAGAA MITANDAONI

Image
Habari zilizosambaa mitandaoni kuhusiana na mabunda ya noti za dola ya Kimarekani kuwa zimekutwa nyumbani kwa mmoja wa watuhumiwa wa mtandao wa wizi bandarini na TRA sio za kweli,  Makubwahaya blog inaweza kuthibitisha.Ukweli ni kwamba mabunda hayo ya noti yalikamatwa huko jijini York, Portland, Marekani Mwezi Septemba mwaka 2010, na sio hapa Dar es salaam, Tanzania kama ambavyo wadau wengi wa mitandao hasa ya Whatsapp na Instagram wanavyovumisha. Tumelazimika kutoa habari hii ili kuokoa wadau wetu wengi katika vuguvugu hili la uvumi wa mitandaoni ambayo hupelekea kazi kuwa ngumu kwa wengi wetu tunaotafuta na kutoa taarifa za uhakika na ukweli. Maana samaki mmoja akioza wote huonekana wameoza. Vile vile hii ni kuwafumbua wale wote wanaohusika kusimamia na kutekeleza sheria ya mitandao wawe macho na kuanza kuchukua hatua madhubuti ili kupunguza kama si kuo

KAULI YA LEMUTUZ KUHUSU KAMISHNA WA KODI TRA KUWA NA NYUMBA 73

Image
Kazi za Magufuli ni kama hizi zinaonekana, watu mnalilia kuongoza tu mmekuwa Viongozi almost maisha yenu yote cha kuonyesha hamna maneno maneno mengi ya ulaghai na ujanja ujanja tulieni muonyeshwe maana ya Uongozi wa Taifa, tulieni muonyeshwe maana ya MABADILIKO huyu mjinga amejijengea nyumba zinazomzidi hata umri wake nyumba 73 hajafikia huo umri lakini tayari ana nyimba kushinda umri wake halafu unamlalamikia Magufuli unalalamika nini? .....mmewafamya.hawa wananchi wajinga for too long tumeimba wote MABADILIKO hapa yamekuja mnaanza kulia lia tena mnalia nini? Tulieni mlikuwa na nafasi ya kuongoza hakuna mlilofanya zaidi ya kila siku kutoa toa zawadi kwa wananchi zolizotokana na mapesa machafu tulikuwa tunajua ila hakuna marefu yasiyokuwa na ncha mwisho wa ujanja ujanja wenu umefika Magufuli hahahaha NAFWAZZZ ....kwa msiyoyajua ya huko ndani Magufuli ni noma sasa hivi sisi wote wananchi mbele yake tupo sawa kamkatalia mpaka Spika aliyetoka kuonana naye kabla uso kwa uso kabla ya u...