Posts

Showing posts from November 27, 2015

;Biashara ya Maduka ya Dawa Baridi Muhimbili Yavurugwa

Image
BIASHARA ya maduka ya dawa baridi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili imeingia shubiri, huku maduka mengine katika hospitali za Serikali yakitakiwa kuwa tayari baada ya agizo la Rais John Magufuli, kuanza kutekelezwa.    Dk Magufuli alipoingia madarakani tu, moja ya maagizo yake alitaka Bohari ya Dawa (MSD) kufungua maduka ya dawa za Serikali kwenye hospitali za rufaa na za kanda, ambapo kesho kutwa Jumatatu duka hilo litaanza kufanya kazi Muhimbili na bei za dawa zitakuwa chini ya bei ya soko. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laureane Bwanakunu, amesema kufunguliwa kwa duka hilo kutaenda sambamba na kufunguliwa na duka lingine katika Hospitali ya Kanda ya Mbeya na baadaye kwenye hospitali zingine za rufaa na kanda na yatatoa huduma mpaka kwa wanaotumia utaratibu wa bima ya afya. Kwa mujibu wa Bwanakunu, pia MSD imeanza kuweka nembo ya Serikali kwenye vidonge na hadi sasa ina vidonge 45 ambavyo vimewekewa nembo ya GOT, ili ...

;Diamond: Sitaki Kabisa Kushika Simu ya Zari Naogopa Kuumia

Image
Diamond Platnumz ameweka wazi kuwa yeye na mpenzi wake Zari ni watu ambao huwa hawapendi kupekuliana simu simu zao ili kuepukana na matatizo yanayoweza kusababishwa na simu za mikononi. Simu za mikononi huwa ni moja ya chanzo cha ugomvi kwa wapenzi wengi, na tumekuwa tukisikia story za couple nyingi kuingia kwenye matatizo kutokana tu na mmoja kukuta ujumbe au picha zenye utata kwenye simu ya mwenzie hata kama haimaanishi kuwa anamsaliti. Diamond na Zari wote ni watu maarufu ambao wana mashabiki wa jinsia tofauti, hivyo kwa kutambua mazingira ya kazi zao wameona ni bora kuaminiana bila kupekuana kwenye simu zao. “Hicho ni kitu cha kwanza ambacho siwezi kudiriki kabisa,” alijibu Diamond alipoulizwa na Millard Ayo kama huwa anashika simu ya Zari. Diamond aliendelea kutoa sababu za kutoshika simu yake, “sidiriki kwasababu namjua ni binadamu , unajua sometimes ukizingatia na yeye (Zari) ni mtu maarufu so sometimes watu wengine wanakuwa wanamsumbua, anaweza kukutwa na vishawishi some...

Waziri Mkuu akutana na hasara ya Bilioni 80 Bandarini

Image
Huko tunakokwenda naona minyukano live.......mie simoooo kazi yangu nafikisha habari tujadiliane.... . . "Siku moja tu ya ziara Waziri Mkuu amekutana na hasara ya Bilioni 80 Bandarini. Hizi ni fedha ambazo zinatosha kuwapa mkopo wa biashara vijana 40,000 wa Kitanzania kila mmoja akapata milioni 2. Pia zinaweza kujenga mabunge mawili yenye hadhi sawa na bunge la Dodoma na zikabaki Bilioni 10 (Bil 35 x 2). Ni fedha ambazo ukiziweka katika noti za elfu kumikumi unaweza kuzitandaza umbali wa kilomita 960 (Bil 80 ÷10,000/= × 12 ÷100,000). Kilomita 960 ni umbali wa kutoka Tunduma hadi Dar. Yani ukatandaza elfu 10 kutoka Tunduma, Mbeya, Makambako, Iringa, Mikumi, Moro hadi Dar bila kuacha hata sentimita moja njiani. Halafu tunaambiwa hii wizara ilikua na Waziri. Tena maWaziri wawili walioitwa maJembe. Mwakyembe na Sitta kwa nyakati tofauti. What a shame?? Majembe wezi? MaJembe ya kupiga dili na watu wa TRA? MaJembe yamekaa wizarani miaka mitano yakashindwa kuona Bil.80 zikipotea, Maj...

Kasi ya Rais Mgufuli, mzigo wa thamani zaidi ya milioni 300 wakamatwa bandarini.

Image
Kutokana na Kasi ya Rais Magufuli yenye motto wa HapaKaziTu, watendaji wa taasisi mbali mbali wameanza kuamka kwenye usingizi wa uzembe na kuanza kufanya kazi. Makontena zaidi ya 30 yamekamatwa yakiwa mbioni kusafirishwa kwenda nchini China yakiwa na mzigo wa magogo kinyume na sheria za nchi. Haijulikana makontena mengine mangapi yamesafirishwa kabla ya haya makontena kukamatwa. It's a new dawn, new day and new life for business as usual!

Sijapenda Majibu ya Msanii wa Diamond Harmonize Kuhusu Mimi- Rose Ndauka

Image
Rose Ndauka Msanii Rose Ndauka amesema kitendo cha msanii Harmonize kujibu majibu yenye utata alipokuwa akihojiwa na kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Televisio, hakupendezwa nacho kwani kinazidi kuleta sintofahamu. Rose Ndauka ameyasema hayo kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, na kusema kwamba Harmonize alitakiwa kujibu moja kwamoja kuwa hawana mahusiano yoyote zaidi ya kufahamiana nae kikazi. “Mi Harmonize namfahamu kama msanii, na hii issue sio mara ya kwanza, tayari nilishaona alihojiwa kwenye interview nyingine alihojiwa kuhusu mimi, what I didn't like ni kwamba angeongea straight, unajua kama huna mahusiano na mtu na ukaulizwa unaongea moja kwa moja, kitendo cha kutengeneza mazingira na watu wakaanza kuweka doubt kwamba Rose na Harmonize watakuwa na mahusiano, hicho ni kitu ambacho mimi sikukipenda”, alisema Rose Ndauka. Rose Ndauka aliendelea kwa kusema kwamba yeye na Haronize hawana mahusiano kama ambavyo H...

Dk. Manyaunyau Ahukumiwa Jela Miaka 3 Kwa Kushindwa Kufufua Maiti

Image
Mkazi  wa Dar es Salaam, Dunia Salumu maarufu kwa jina la Dk. Manyaunyau, amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela pamoja na kulipa fidia ya Sh milioni 10 baada ya kupatikana na hatia ya kujipatia fedha Sh milioni 29.6 kwa njia ya udanganyifu. Manyaunyau anadaiwa kujipatia kiasi hicho cha fedha kutoka kwa mlalamikaji, Tekra Modesta kama malipo ya kazi ya kumfufua marehemu kaka yake aliyefahamika kwa jina moja la Modest ambaye alifariki dunia miaka kadhaa iliyopita. Akitoa hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, Flora Haule, alisema mtuhumiwa huyo ametiwa hatiani baada ya ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashtaka kujitosheleza. “ Mahakama inatoa hukumu kwa mtuhumiwa kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela na kulipa fidia ya Sh milioni 10 baada ya kumaliza kutumikia kifungo chake ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hizo, ” alisema Hakimu Flora. Upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi wanne ambao wote waliithib...

Marekani Yaipa Kibano Tanzania .....Yaitaka Serikali itoe Maelezo Uchaguzi Zanzibar na Sheria ya Mtandao , Yatishia kusitisha Msaada wa Trilioni

Image
Mfuko wa Changamoto za Milenia (MCC) wa Marekani umeonya kuwa hali ya kisiasa Zanzibar na tukio la hivi karibuni la watu kukamatwa chini ya sheria mpya ya uhalifu mtandaoni yanaweza kuathiri vigezo vya kuiwezesha Tanzania kupata msaada. Katika barua ya MCC ya Novemba 19, ambayo imesainiwa na Naibu Makamu wa Rais wa Idara ya Operesheni ya Miradi kwa Afrika, Jonathan O. Bloom kwenda kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dk. Servacius Likwelile, mfuko huo umetaka maelezo kuhusu utatuzi wa mgogoro wa Zanzibar pamoja na ufafanuzi wa sheria ya uhalifu wa mtandaoni. “MCC inashukuru kwa uongozi na dhamira yako wakati wa mchakato mzima wa maendeleo ya mradi huu. Msaada wa dola milioni 472 (ambazo ni zaidi ya Sh trilioni moja), una nafasi kubwa ya kusaidia kuleta mageuzi katika sekta ya nishati na kuwaunganisha maelfu ya watu katika gridi. “Lakini mgogoro wa Zanzibar na ukamataji watu wa hivi karibuni kupitia sheria mpya ya uhalifu mtandaoni umetutia wasiwasi. “Kama ujuavyo, mataifa wa...

Kubenea Aibua Ufisadi wa Billion 1.2 Kupitia Ufuaji wa Majoho ya Madiwani

Image
MBUNGE wa jimbo la Ubungo, Saed Kubenea ameibua ufisadi wa Shilingi bil. 1.2 kwa mwaka katika Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam unaofanywa kupitia ufuaji wa majoho ya madiwani. Kubenea amesema hayo Stendi Kuu ya mabasi yaendayo mikoani alipofanya ziara ya siku moja kutembelea soko la Urafiki maarufu kama Mahakama ya ndizi, soko la Mabibo na kuhitimisha ziara yake katika Stendi za Ubungo na Simu 2000 “Baada ya kufanya uchunguzi tumebaini kuwa mradi huo wa ufuaji majoho kabla ya madiwani kufanya kikao unaotumia shilingi bilioni 1.2 hivyo basi Halmashauri ya Manispaa itakayokuwa chini ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) tukianza kazi tutaufuta,” alisema Kubenea. Aliongeza kuwa kufutwa kwa mradi huo kutafanywa mara moja baada ya Ukawa kupata Meya wa Manispaa na Jiji kutokana na ukweli kwamba wana Halmashauri mbili kati ya tatu hivyo zitawawezesha kumpata Naibu Meya katika Chama Cha Wananchi (CUF) na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Kubenea alisema jambo jing...

Breaking News:Waziri mkuu Majaliwa avamia bandari leo, aamrisha kukamatwa kwa maafisa kibao wa TRA

Image
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akikabidhi orodha ya makontena yaliyopotea na ambayo TRA haina taarifa nazo Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa leo ameamuru kukamatwa kwa maafisa kadhaa wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na wengine kufukuzwa kazi baada ya kufanya ziara ya kushtukiza Bandarini na kukuta madudu ambayo hakuyafurahia. Maafisa hao, ambao kwa sasa tunahifadhi majina ili Jeshi la Polisi liweze kuwashughulikia, wametakiwa pia kusalimisha hati zao za usafiri. Hii imekuja baada ya kugundulika kwamba kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya Bandari inazo lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani.

Bunge Kuondoa Ajira za Kudumu Serikalini.....Kudumu Kwa Ajira Ya Mfanyakazi Kutategemea Juhudi Zake Kazini

Image
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania litafanyia mabadiliko makubwa sheria za utumishi wa umma kwa kuondoa ajira za kudumu serikalini, ili kuwezesha mabadiliko yaliyokusudiwa na Rais Dk. John Magufuli. Katika mabadiliko hayo, mfumo sasa wa ajira za serikali kuwa za kudumu utabadilishwa na badala yake, kudumu kwa ajira ya mfanyakazi kutategemea juhudi na bidii yake kazini, ili kuondoa uzembe uliodumu miaka nenda miaka rudi, katika sekta ya umma. Akizungumza katika mahoajino binafsi na gazeti la  Raia Mwema, mjini Dodoma mwishoni mwa wiki iliyopita, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai, alisema baadhi ya sheria za kazi zinawafanya baadhi ya watumishi wa umma kuwa wazembe. “ Kwa mfano katika serikali ya sasa mfanyakazi mzembe kabisa kabisa hata waziri kumfukuza kazi hawezi. Hata Katibu Mkuu hawezi mpaka afuate mlolongo mrefu na hatua nyingi sana, yaani kazi ni guarantee (uhakika) katika nchi yetu ni permanent and pensionable (ya kudumu na in...

Tamasha kubwa la burudani la INSTAGRAM PARTY kufanyika Jumamosi viwanja vya Escape One Mikocheni jijini Dar

Image
Mkurugenzi Mtendaji  wa Freconic ideaz, Fred Ngimba akifafanua jambo alipokuwa anaongea na waandishi wa habari jana katika fukwe za Escape One kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya tamasha kubwa la burudani litakalofanyika jumamosi hii  tarehe 28 ,kulia kwake ni Meneja mawasaliano wa Freconic ideaz Krantz Mwantepele  Mmoja wa wadau akitembelea ukurasa wa INSTAGRAM  PART  TZ kupata taarifa mbalimbali kuhusu tamasha hili litakalowakumbusha wapenzi wa burudani nyimbo za zamani ,misemo ya zamani hata mavazi ya zamani kukiwa na kauli mbiu ya BONGO THROW BACK  Mkurugenzi wa Freconic ideaz, Fred Ngimba (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu tamasha kubwa la burudani la Instagram Party litakalofanyika Jumamosi katika viwanja vya Escape One Mikocheni likiwa na kauli mbiu Bongo Throw Back. Kulia ni Meneja Mawasiliano, Krantz Mwantepele. Wanahabari wakichukua taarifa hiyo. Wanahabari wakiwa ...

Serikali Yakanusha Hazina Kuachwa Tupu Bila Fedha na Rais Kikwete

Image
Serikali imekanusha taarifa zinazosambazwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa Rais mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa amekomba fedha hazina na kuiacha Serikali bila fungu lolote. Hayo yamesemwa jijini dare es salaam na Kamishina wa Bajeti kutoka Wizara ya Fedha Bwa. John Cheyo huku akiwataka wananchi kupuuza habari hiyo kwani hazina ukweli wowote. “Hazina inazo pesa za kutosha  na tunajivunia kufanya uchaguzi wa mwaka huu,  kununua mashine za BVR  kwa kutumia pesa za watanzania bila kutegemea msaada wowote kutoka nje ya nchi  na kutoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu mwaka huu” alisema Bwa. Cheyo. Pia aliongeza kuwa serikali imeendelea kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa bomba la gesi ambalo limekamilika hivi karibuni, vinu vya kuchakata gesi na ujenzi wa barabara nchini. Aliendelea kusema kwamba mfumo wa serikali wa bajeti unaiwezesha serikali kupanga vipaumbele vya matumizi kulingana na bajeti ilivyopangwa ambap...

BEN POL: "COKE STUDIO NI HATUA KUBWA KWANGU KIMUZIKI"

Image
Msanii wa muziki wa kizazi kpya nchini,Benald Paul ‘Ben Pol’ amesema ushiriki wake katika onesho la Coke Studio ni moja ya mafanikio katika safari yake ya muziki.  Kauli hiyo aliitoa wiki hii kuhusu ushiriki wake kwenye onesho hilo linaloendeshwa na kampuni ya CocaCOla kwa kushirikisha wanamuziki wa Tanzania na nje ya nchi ambao wamekuwa wakifanya onesho la kuvutia.  alisema anajivunia ushiriki wake katika maonesho hayo na amefanikiwa kujifunza mengi kuhusu fani ya muziki.  Alisema anajisikia fahari kufanya kolabo kwa kushirikiana na wanamuziki wengi kutoka Kenya katika msimu huu wa Coke studio ambapo kwa hapa nchini onesho hilo linarushwa kila Jumamosi.  Ben Pol alisema onesho ka Coke Studio linahamasisha vijana kujiamini na kuonesha vipaji vyao na aliwataka vijana wenzake kujiamini na kutokata taaa iwapo wataka kutimiza ndoto zao na kufanikiwa katika maisha.