MKE WA SLAA AJIBU MAPIGO YA GWAJIMA
MKE wa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), Dk. Willibrod Slaa, Josephine Mushumbusi, ambaye amekuwa akitupiwa tuhuma nyingi za kumponza na kumsababishia aibu mume wake amesema kuwa hajaona jambo lolote lenye maudhui ya kujibu tuhuma zinazoelekezwa dhidi yake. Kauli hiyo ya Mushumbusi imekuja siku chache baada ya Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima ambaye Dk. Slaa alimtaja kama mshenga wa tukio la Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kujiunga na Chadema, kudai ana ushahidi unaoonyesha kuwa mama huyo ndiye chanzo cha mume wake kuacha siasa. Mushumbusi ambaye yuko nje ya nchi, alitoa msimamo huo katikati ya wiki hii wakati akiwasiliana na MTANZANIA Jumamosi kwa njia ya barua pepe. Amejipambanua kwa kusema kwamba mafanikio yake yataonekana muda si mrefu hivyo kwa sasa amefunga mikono. “You will see ...