Posts

Showing posts from September 19, 2015

JESHI LA POLISI SASA WANAMSAKA "DAUDI BALALI" NI YULE ALIYEWAHI KUWA GAVANA WA BENKI KUU BOT ...WAAHIDI KUMPAT

Image
Jeshi la Polisi nchini linafanya uchunguzi kumbaini mmiliki wa ukurasa wa twitter unaoendeshwa na anayejiita Daudi Balali, aliyewahi kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake. Mkurugenzi wa Habari na Mahusiano wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba, aliyasema hayo wakati akizungumza na Nipashe ofisini kwake jana. Bulimba alisema kuwa taarifa za uwapo wa ukurasa huo wa twitter, wamekwishazipata na wanafanya uchunguzi wa kina kumkamata mhusika kisha kumfikisha kwenye vyombo vya sheria. “Tunazo taarifa juu ya ukurasa huo wenye wafuasi wengi kwa sasa na unaotumika kuwashambulia viongozi wa serikali na wa siasa hasa wale wanaogombea nafasi kubwa za utawala nchini, hivyo Jeshi la Polisi lipo kwenye uchunguzi ili kumbaini mtu huyo haraka iwezekanavyo,” alisisitiza Senso. Ukurasa huo ulioanza kutumika kabla ya Sheria ya Uhalifu wa Mtandaoni kuanza kutumika, una wafuasi zaidi ya 6,000 kwa sasa na umekuwa ukitumika kuwachafua wag...

BREAKING NEWZ:SASA MAREKANI YATOA ANGALIZO UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA..SOMA KAULI YAO HAPA KALI

Image
Siku moja tu baada ya Umoja wa Ulaya (EU) kutabiri kuwapo kwa ushindani mkali katika uchaguzi mkuu nchini utakaofanyika Oktoba 25, Serikali ya Marekani imeibuka pia na kutoa angalizo kuhusiana na uchaguzi huo unaohusisha wagombea urais saba wakiwamo Dk. John Magufuli wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Edward Lowassa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na Shirika la Changamoto za Milenia (MCC) linalomilikiwa na Serikali ya Marekani kwa ajili ya kusaidia nchi zinazoendelea, ilieleza kuwa Bodi ya MCC ina matumaini uchaguzi mkuu wa Tanzania utakaofanyika Oktoba 25 utakuwa huru na wa haki, hasa ikizingatiwa umuhimu mkubwa ambao MCC inauweka katika haki za kidemokrasia.  Kadhalika, taarifa hiyo imemkariri Balozi wa Marekani nchini, Childress akisema (Marekani) wanatambua rekodi ya Tanzania katika kukuza demokrasia na kwamba, wanaunga mkono na kusaidia jitihada endelevu za Tanzania katika kuimarisha ...

Millen Magese apoteza fahamu mara mbili katikati ya jiji la New York

Image
Mwanamitindo na Miss Tanzania wa zamani, Happiness Millen Magese alipoteza fahamu mara mbili katikati ya jiji la New York nchini Marekani. Kupitia Instagram, Millen amesema ni msamaria mwema ndiye aliyemsaidia. “ Something happened this afternoon right after I posted my last video,which reminded me a very important thing we always forget,” aliandika. “ Every one of us will go and it’s just a matter of time ,be ready all the times ,I passed out twice on 42 street in New York today ,and strangers helped me. #Lesson -Help somebody anywhere they need. [pray] #I wish to meet these two guys who helped me. Especially the one who carried me a cross to my building. God bless you .” “ Iam Alive . Am Ok . Thankful #Thank you @funminewyork and #mimabuilding #ItIsWell. All in Control. [pray] .” Tupe maoni yako hapo chini

Mke Halali wa DR SLAA Ajitokeza Akiwa na Watoto Halali wa Slaa na Kumchana Slaa na Kudai Ametumwa na CCM

Image
Mbunge wa Viti    Maalumu kupitia chadema,Rose Kamili,akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo jioni kuhusiana na tuhuma alizozitoa mume wake kwamba waliishi kwa maisha ya kula mihogo na familia yake ili kuhakikisha chadema inastawi na kuimarika jambo ambalo si la kweli walikuwa na maisha mazuri ya kawaida tu na kusema kuwa Dk.Slaa anapaswa awaombe radhi wataznzania kwa kufafanisha kula mihogo kuwa ni umaskini na kuongeza kwa kusema mbona ukienda katika mahoteli makubwa mihogo na viazi ipo na watu wenye pesa zao wanakula kama kawada. akizungumzuia kuhusu matamshi aliyasema Dk.Slaa kwamba haongei na waziri mkuu mstaafu,Sumaye,mama rose kamili alisema kuwa wiki tatu zilizopita waziri mkuu huyo mstaafu aliomba namba za dk.slaa akampatia wakaongea vizuri bila shida yoyote ila anamshangaa juzi aliposema mbele ya waandishi wa habari kwamba hazungumzi na sumaye. akizungumzia kuhusu kuja kwa lowassa chadema mama huyo alisema kuwa Dk.slaa alikuwe...

Mabango ya Lowassa yazua kizaazaa

Image
MABANGO yenye picha ya mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, yanayoendelea kubandikwa katika maeneo mbalimbali nchini yamezua kizaazaa, baada ya mengine kuondolewa na wale wanaofanya kazi ya kuyaweka kutishwa na hata kuwekwa ndani na Jeshi la Polisi. Hali hiyo imejitokeza mkoani Iringa, ambako vijana wanaofanya kazi ya kuweka mabango hayo waliwekwa ndani na Jeshi la Polisi na jijini Dar es Salaam ambako bango lililokuwa limewekwa katika Soko la Kariakoo liliondolewa saa chache tu baada ya kubandikwa na hivyo kuzua mjadala kila kona. Wakati wale waliokamatwa mkoani Iringa wakidaiwa kuwekwa ndani pasipokuwa na sababu yoyote hadi pale walipotolewa na maofisa wa Chadema, Jijini Dar es Salaam bango hilo liliondolewa na uongozi wa Soko la Kariakoo kwa madai ya kubandikwa kimakosa. Juzi saa 12 jioni wafanyakazi wa kampuni ya Platnum Media Co. Ltd walifika sokoni hapo na kuanza kubandika bango hilo lililokuwa n...

Picha: Hatimae Jacqueline Wolper Avishwa Pete ya Uchumba

Image
Mwezi mmoja toka Jacqueline wolper atamke kuwa ni mjamzito (ambao bado haujapata uthibitisho-Ingia  hapa ), mrembo huyo wa Bongo movie amevishwa pete ya uchumba. Kwa mujibu wa picha na maelezo aliyopost kwenye akaunti yake ya Instagram, Wolper sasa ni mchumba wa mtu. Wolper alipost picha kadhaa akiwa na mchumba wake, na kuelezea picha kamili ilivyokuwa hadi kupata surprise hiyo ambayo hakuitarajia. Baada ya maelezo hayo yaliyofatiwa na picha za tukio lenyewe, pongezi nyingi zimemwagika kutoka kwa followers wake. Hizi ni baadhi ya comments; annietzdu : Nakupongeza kwa kutochukua mtu maarufu mungu awatangulie sana mtimize lengo lenu mmeendana sana new_isha : Usiishie Pete ndoa fastaaa my nduguuuu love uuuu na unialike mwezimbili : Hongera kaka kwan umembadilisha tabia Dada Jack.hususanani ktk mavazi Mungu amibariki.Dada Jack jitambue kuna ile SKU moja utakua mama hivyo basi heshima ndio nguzo pekee ktk masha hebu onyesha mfano. beibycso :...

Askofu Gwajima Amjibu DR Slaa..Baada ya Kumtuhuma Makubwa na Kumwita Mshenga

Image
Askofu Josephat Gwajima amejibu tuhuma zilizoelekezwa kwake na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa kuwa alishiriki kama ‘mshenga’ kumshawishi mwanasiasa huyo kumpokea Edward Lowassa katika chama hicho. Jana, Dk. Slaa alimtaja Askofu Gwajima kama mshenga na kwamba alimshawishi ampokee Lowassa huku akidai kuwa askofu huyo alimtamkia kuwa maaskofu 30 wa Kanisa Katoliki walihongwa na timu ya Lowassa.   Askofu Gwajima amekanusha taarifa zilizotolewa na Dk. Slaa ambaye alikuwa rafiki yake kwa muda mrefu akidai kuwa ni muongo mkubwa. Alisema kuwa Dk. Slaa ameamua kuwashambulia maaskofu hao kwa kuwa anafahamu hawana majukwaa ya kumjibu kama ilivyo kwa wanasiasa. Gwajima alidai kuwa yeye aliitwa kama msuluhishi ndani ya Chadema na sio mshenga wa kumleta Edward Lowassa.   “Kwa kawaida inashangaza kwamba kama watu wawili wanagombana inatakiwa awepo mtu wa kuwaunganisha, ila anaposema maaskofu 34 haileti maana, haiingii akili, ameingiza Gwaj...