Posts

Showing posts from November 25, 2015

Mimba ya Jokate Yazua Balaa, Familia Yashtuka

Image
Kwani kimenuka? Siku chache baada ya kubumburuka kwa habari ya kunasa mimba ikimhusisha ‘mtoto mzuri’ Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ huku mhusika mkuu akitajwa kuwa ni msanii nguli wa Bongo Fleva, Ali Kiba, ishu hiyo imezua balaa kufuatia familia ya mrembo huyo kushtushwa na hali hiyo, Ijumaa Wikienda limenyetishiwa. TWENDE OYSTERBAY Mwishoni kwa wiki iliyopita, ‘kijumbe’ wa gazeti hili alitua getini nyumbani kwa akina Jokate, Oysterbay jijini Dar kwa lengo la kutaka kujua nini kinaendelea juu ya binti yao kunasa mimba nje ya ndoa ilihali familia hiyo inasifika kwa misingi bora na maadili ya kidini. Gazeti hili lilipotia timu nyumbani hapo, lilifanikiwa kuzungumza na mmoja wa wanafamilia hiyo aliyekuwa nje akifanya usafi ambaye bila simile ‘alifunua kinywa’ na kuweka hadharani mambo mazito. GAZETI LA IJUMAA LAIBUA MAMBO Kama anayeogopa jambo fulani, memba huyo wa familia ya Jokate alisema kuwa, mrembo huyo alikuwa akifanya siri kubwa juu ya ujauzito wa...

Kaka Hana Uwezo wa Kupata Mtoto, Je Naweza Kumsaidia Kumpa Mkewe Ujauzito?

Image
Najua hapa kuna wenye ujuzi na hekima na busara. Hoja ni jee ikiwa kaka yangu wa baba na mama mmoja ana mke, na ameishi nae kwa miaka zaidi ya tisa lkn hawajapata mtoto. ila huyu mwanamke ana mtoto aliempata kwa mnmumewingine kabla ya kuolewa na kaka mimi nimeoa miaka sita ilopita na tayari mke wangu ana watoto wawili. Sasa ktk ndoa ya kaka tayari kuna minong'ono kuwa kaka ndie tatizo maana jamaa hajawahi hata kusingiziwa mtoto mitaanirafiki wa familia yetu mmoja amenishauri nifanye mpango wa siri na shemeji ili ikiwezekana nihakikishe anapata uja uzito uhusiano wangu na shemeji yangu ni mzuri na niwakaribu. na mara nyingi tunapotoka na wife huongozana nae kwasababu ya majukumu yake. Je, naweza kukubali ushauri huo kwa siri ili kurejesha amani ya kaka? Lakini ili kulinda heshima ya familia yetu, inabidi angalao shemeji atuletee mtoto. Wandugu, niambieni naweza kumsaliti kaka kulinda heshima ya familia

Kasi ya Magufuli Yamzindua Usingizini Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.....Nae Awapiga Chini Mawaziri Wote Wenye Kashfa Za Ufisadi

Image
Uhuru Kenyatta Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amefanya mabadiliko katika Baraza la Mawaziri na kuwapiga chini mawaziri wote ambao wizara zao zinakumbwa na kashfa za ufisadi. Uamuzi wa Rais Kenyatta umekuja siku moja baada ya kutangaza ufisadi kama tishio la usalama wa kitaifa huku akiazimia kufanya mabadiliko makubwa kwenye ofisi ya Rais hivi karibuni. Katika mabadiliko hayo, Kenyatta ameongeza pia idadi ya wizara kutoka 16 hadi 20 na kuongeza idara mpya chini ya wizara hiyo, kutoka idara 26 hadi 41 kwa kile alichoeleza kuwa ni kusaidia wizara kutekeleza majukumu yao bora zaidi. Baadhi ya mawaziri walikuwa tayari wamekwisha jiondoa kwenye wizara zao kwa tuhuma za ufisadi huku wengine wakiwa na kesi za kujibu mahakamani. Hivi karibuni, Waziri wa Ugatuzi, Anne Waiguru alikuwa wa mwisho kujiondoa kwenye wizara akiwa na kashfa zilizopata umaarufu zaidi kwa kipindi cha hivi karibuni za kununua kalamu moja kwa shilingi zaidi ya 200,000 za Tanzania. Hata ...

MAAJABU YA DUNI;Mwafrica wa kiume aolewa Marekani

Image
matatizo ya demokrasia kuzidi Habari hii ni moja ya vielelezo vingi kuthibitisha ni kiasi gani tumefikia pabaya..Malezi ya mtoto wa kiume yamekuwa yenye tension kubwa siku hizi kuliko hata wa kike,na shida ni wazazi hawa wa .com parents have no time for their kids, nannys our nowadays mothers. a mom/dad doesn't know about her/his kid's home works, kid's favourite subject, the challenges a kid faces at school etc. only the nanny/houseboy knows well of the kid. there is no more parental guidance on some tv programs on wat to watch etc we say we living in a digital life. a son can take dad's car n gout with friends n come back late night without dad' asking. what do you think its the result?  Single parent families pia ni chanzo ..N hili swala la baba  Kushindwa kulea watoto wetu wa kiume kwa karibu katika misingi ya imani na maadili yanapelekea wao kupotea, Baba kama kichwa cha familia anatakiwa awe mfano, mtoto wa kiume akue akimwona baba yake kama...

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Awasweka Rumande Maofisa Ardhi 10 Kwa Masaa 6

Image
Hatutaki uzembe awamu ya tano Paul Makonda Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda leo amewaweka ndani kwa saa sita maofisa ardhi zaidi ya 10 huko Kawe baada ya kuchelewa kufika eneo walilokubaliana kukutana. Makonda jana alikuwa amewataka Maofisa hao  kufika eneo la Nakasangwe Kata ya Wazo leo asubuhi kutoa ufafanuzi wa mgogoro wa ardhi lakini wao wakafika saa 5.

Mtoto wa Alphonce Mawazo Akiwa na Lowasa Alipotoka Kufanya Mtihani wa Taifa Leo

Image
Mtoto wa Kamanda wangu Alphonce Mawazo akiwa na Mhe Edward Lowasa alipotoka kufanya Mtihani wake wa Taifa wa darasa la Nne Tuko pamoja mtoto wa Rafiki yangu PreciousAlphonceMawazo

Vikwazo Vitano Vyatajwa Kwenye Agizo la Rais Magufuli Kufuta Safari za Nje

Image
Agizo la Rais John Magufuli la kusitisha safari za nje linakabiliwa na ugumu katika utekelezaji wake kutokana na nchi kuwa na balozi 36 tu ambazo zitatakiwa kufanya kazi maeneo mbalimbali duniani. Muda mfupi baada ya kuapishwa na kuanza utekelezaji wa majukumu yake ya mkuu wa nchi, Rais alifuta safari zote za nje kwa watumishi wa Serikali na viongozi ili kuokoa fedha zinazotumika kwa ajili hiyo na kuagiza shughuli hizo zifanywe na mabalozi. Rais alisema safari hizo zitadhibitiwa na Ikulu ambayo itatoa kibali kwa safari maalumu, ikiwa ni pamoja na kuweka masharti ambayo mtumishi anayetakiwa kusafiri atatakiwa kuyatimiza kabla ya kupewa kibali. Lakini utekelezaji wa agizo hilo unakabiliwa na vikwazo vingi, hasa vikubwa vitano ambavyo ni uchache wa balozi za Tanzania nje ya nchi, ukomo wa madaraka ya mabalozi, wigo wa ufahamu wa mambo ya kitaalamu na ukosekana kwa mazungumzo endelevu iwapo suala moja litawakilishwa na watu wawili tofauti kwenye mikutano miwili tofa...

Ziara ya Papa Francis!! Hivi ndivyo Wakenya walivyomkaribisha leo..+Pichaz

Image
Papa Francis wa kanisa katoliki duniani ameanza ziara yake katika nchi za Afrika na leo alikuwa Kenya. Papa Francis alilakiwa na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta katika uwanja wa ndege uliopo Nairobi na kuwashukuru Wakenya kwa kumkaribisha vizuri huku akiwatakiwa baraka tele za Mwenyezi Mungu. Nchi nyingine za Afrika ambazo Papa Francis atatembelea ni pamoja na Uganda pamoja na Jamuhuri ya Afrika ya Kati.

MFAHAMU STAA WA JUMONG..SONG II GOOK.

Image
Wengi wanamfahamu kama jumong au Peter pan katika tamthilia ya A MAN CALLED GOD.Anaitwa SONG II GOOK kitukuu wa kiongozi wa waapigania uhuru wa korea kusini.alizaliwa mwaka 1971 mosi oktoba.mama yake pia alikuwa mwigizaji.   Ni muhitimu wa elimu ya juu katika chuo kikuu cha cheongju university katika masomo ya sanaa.MWAKA 2008 alifunga ndoa na asubuhi ya tarehe 26 mwezi wa tatu 2012 mkewe alijifungua watoto watatu.aliwaita majina ya DAE HAN,MIN GUK na MAN SE ambayo ukiyatamka kwa pamoja humaanisha MAISHA MAREFU KWA JAMHURI YA KOREA.Kwa sasa yeye na familia yake wanaonekana kwenye tamthilia ya THE RETURN OF SUPER MAN.mwaka 2004 aliigiza empor of the sea,2006 alicheza jumong,2008 ni land of wind na 2010 ni   A MAN CALLED GOD. HAPA CHINI NI LIST YA TAMTHILIA ALIZOCHEZA Filmography TV series Year Title Role Network 1999 Did We Really Love? MBC Goodbye My Love MBC ...