MAGAIDI WALIJIFANYA WAHAMIAJI:UFARANSA

Waziri Mkuu wa Ufaransa Manuel Valls.
Waziri mkuu wa Ufaransa,Manuel Valls, amesema kwamba watu wanaohusishwa na kundi la Islamic State ambao walitekeleza shambulizi mjini Paris wiki iliyopita,ambalo liligharimu uhai wa watu mia moja na ishirini na tisa,waliingia nchini humo kwa mgongo wa sakata la uhamiaji barani ulaya na kuzamia nchini Ufaransa bila kugundulika.
Ameyasema hayo wakati alipokuwa anazungumza katika runinga ya taifa hilo na kwamba wahusika wengine wa ugaidi walikuwemo katika nchi za Ufaransa na Ubelgiji mapema.
Waziri huyo aliongeza kuwa haikufahamika mara moja kwamba kulikuwa na makundi ya namna hiyo kwa ukubwa wake ,ama mshukiwa Salah Abdeslam, ambaye ndiye hasa kielelezo cha mwanamume anayesakwa zaidi kimataifa na haikujulikana kama alikuwa Ubelgiji ama Ufaransa.

Comments

Popular posts from this blog

Ang'atwa na Nyoka Akizini na Mke wa Mtu Kichakani

Kubenea Aibua Ufisadi wa Billion 1.2 Kupitia Ufuaji wa Majoho ya Madiwani

Tundu Lissu Ajibu Mapigo.......Asema Mwenye Richmond ni Rais Kikwete Mwenyewe